Baada ya kukosa penati na Argentina kushindwa kutwaa kombe la Copa America, mchezaji nyota Lionel Messi amechukua uamuzi mgumu wa kujiuzulu kuichezea tena timu ya taifa.

Ni kwa miaka tisa mfululizo Argentina imejikuta ikipoteza nafasi ya kutwa kombe mara nne katika michuano ya kimataifa, huku Messi akishindwa kuisaidia kabisa.

Messi akiwa na Argentina amefanikiwa mara moja tu kutwaa medali ya dhahabu katika michuano ya Olimpiki.

Lakini akiwa na klabu yake ya Barcelona Messi ameshinda ubingwa wa Ligi ya Kuu ya Hispania 'La Liga' mara nane na Ligi ya Mabingwa Ulaya mara nne. 

Lionel Messi akipiga mkwaju wa penati aliyoikosa na kuamua kufanya maamuzi magumu.

Post a Comment

 
Top