Hofu na wasi wasi umezidi kutanda  mkoani Dodoma baada ya kuibuka kwa ugonjwa usiojulikana.
 

Hadi sasa jumla ya watu saba wamefariki na wengine 21 kulazwa katika hospital ya mkoa mjini Dodoma baada ya kuzuka ugongwa huo ambao hadi sasa madaktari haujui tiba yake.
Dalili za ugonjwa huo ni pamoja na kutapika, kuharisha, ngozi na macho kuwa ya njano pamoja na kuumwa na tumbo.
Kufuatia kuibuka kwa ugonjwa huo tayari kumetengwa wodi maalum katika hosptali ya taifa ya rufaa ya Dodoma ambapo pia karantini imewekwa na hakuna anayeruhusiwa kukaribia mahali hapo zaidi ya madaktari ambao nao pia wanaingia kwenye wodi kuwaona wagonjwa kwa tahadhari kubwa.

Post a Comment

 
Top