Laurent Fabius
Waziri wa mashauri ya kigeni nchini Ufaransa Laurent Fabius ameelezea hisia za baadhi ya nchi za ulaya dhidi ya suala la uhamiji kuwa sawa na sakata.
Amezilaumu nchi za ulaya hasusan zilizo mashariki mwa ulaya kwa kukataa kuwaruhusu wahamiaji.
 
Wahamiaji kwenye mpaka wa Hungary na Serbia
Bwana Fabius aliiilaumu Hungary kwq kujenga ua ulio na lengo la kuzuia watu wanaowasili wakipitia nchini Serbia akisema kuwa hatua hiyo haiendi sawa na maadili ya ulaya.
Ufaransa imejiunga na Uingezea pamoja na na Ujerumani katika kuitisha mkutano wa dharura na mawaziri wa nchi za ulaya kutafuta njia za kukabiliana idadi ya wahamiaji inayozidi kuongezeka.

Post a Comment

 
Top