Bunge la Israeli limetupilia mbali sheria za kuvaa kwa wafanyakazi wa bunge baada ya wafanyakazi hao kupinga sheria zinazowataka kutovalia sketi fupi.
Wafanyajazi hao walidai kuwa walinzi katika bunge walikuwa wakitekeleza sheria hizo na kuwazuia watu kuingia bunge hilo.
Spika Yuli Edelstein alisema kuwa hatua hiyo ilichukuliwa baada ya malalamiko kuhusu mavazi yasiyoridhisha.
Sasa timu itateuliwa kuangalia vile sheria hizo zitatatekelezwa.
Mwezi Oktoba usimamizi wa bunge ulituma barua kuwakumbusha wafanyakazi wote wa bunge kuhusu sheria hiyo ya mavazi.

Post a Comment

 
Top